Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian tarehe 22.07.2022 amefungua kikao cha robo mwaka cha kujadili takwimu za UKIMWI na chanjo ya UVIKO-19 kwa timu ya Afya ya Mkoa, timu za Afya za Halmashauri 8 za Mkoa wa Tabora na Wadau wa Afya ( MDH)
![](https://www.mzawa.co.tz/wp-content/uploads/2022/07/IMG-20220723-WA0031.jpg)
Wakati wa ufunguzi, Mkuu wa Mkoa ametoa maagizo na maelekezo ya kusimamia utoaji wa Huduma za Afya vizuri ili kuendelea kuboresha Afya za wananchi wa Mkoa wa Tabora.
![](https://www.mzawa.co.tz/wp-content/uploads/2022/07/IMG-20220723-WA0032.jpg)
Aidha, Mhe. Mkuu wa Mkoa ametoa vyeti vya pongezi kwa wadau wa MDH na Halmashauri za Mkoa wa Tabora kwa kufanya vizuri katika chanjo ya UVIKO-19 na kufanya Mkoa wa Tabora kuwa wa kwanza Kitaifa.
![](https://www.mzawa.co.tz/wp-content/uploads/2022/07/IMG-20220723-WA0029.jpg)