Home Kitaifa MIAKA 25 YA CHUO CHA UTUMISHI WA UMMA TANZANIA, MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA...

MIAKA 25 YA CHUO CHA UTUMISHI WA UMMA TANZANIA, MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA KUJENGA RASILIMALIWATU YENYE TIJA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Viongozi mbalimbali, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akiteta jambo na Katibu Mkuu wa ofisi yake Bw. Juma Mkomi (kulia) wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Menejimenti, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akifurahia jambo na Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu, Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Dkt. Ernest Mabonesho (kushoto) wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao kwenye hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Menejimenti, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Na. Veronica Mwafisi-Dar ES Salaam 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) ina nafasi ya kipekee katika kujenga na kuendeleza uwezo wa kiutendaji wa watumishi wa umma ambao ndio watekelezaji wa majukumu ya Serikali kila siku.

Waziri Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 03 Julai, 2026 wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya TPSC yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Kikwete amesema, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuweka kipaumbele katika uimarishaji wa Utumishi wa Umma ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, za haraka na zenye tija. 

Mhe. Kikwete ameongeza kuwa, Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania si tu taasisi ya mafunzo, bali ni nguzo muhimu ya Serikali katika kujenga rasilimaliwatu yenye maarifa, stadi, maadili na uzalendo unaohitajika katika kutumikia umma kwa ufanisi.

Katika hatua nyingine, Mhe. Kikwete amesema kuwa, Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inatutaka kuwa na Taifa lenye uchumi wa kisasa, ushindani wa kimataifa, matumizi makubwa ya teknolojia, na huduma za umma zenye ufanisi wa hali ya juu. Hivyo, mafanikio ya Dira hiyo yatategemea kwa kiasi kikubwa uwepo wa watumishi wenye sifa, ujuzi na uwezo wa kuongoza mabadiliko hayo. 

“Chuo hiki kina wajibu mkubwa wa kuhakikisha  Watumishi wa Umma wanapata maarifa na stadi zinazolingana na mahitaji ya karne ya ishirini na moja ili kuwepo wa watumishi wenye sifa, ujuzi na uwezo wa kuongoza mabadiliko hayo,” amesema Waziri Kikwete.

Aidha, Mhe. Kikwete amewapongeza watangulizi wake kwa usimamizi mzuri ambao umechangia mafanikio makubwa ya Chuo hicho huku akimshukuru Katibu Mkuu wa Ofisi yake, Bw. Juma Mkomi kwa kuendelea kusimamia Chuo hicho kiutendaji. 

Vilevile, Waziri Kikwete ameipongeza Bodi ya Ushauri ya TPSC, Menejimenti, Watumishi, Wanafunzi na wadau wote kwa mchango wao katika safari ya kutimiza miaka 25 ya mafanikio ya chuo hicho.

Akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mhe. Waziri kuzungumza na wadau katika hafla hiyo, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi ametoa wito kwa waajiri kutumia Kampasi za TPSC zilizo katika kanda zao ili kuwawezesha watumishi ikiwemo waajiriwa wapya kupata mafunzo ya awali.

“Kampasi katika Kanda hizo zimewekwa kimkakati ili kusogeza huduma za chuo katika mikoa mbalimbali, hivyo Waajiri wazitumie kikamilifu kwa watumishi kupata mafunzo kwa lengo la kuboresha utendaji kazi.” Amesisitiza Katibu Mkuu Mkomi.

Amezitaja Kampasi hizo kuwa ni Dar es Salaam, Mbeya, Tanga, Singida, Tabora na Mtwara na kuongeza kuwa Ofisi ya Rais-UTUMISHI itaendelea kuunga mkono jitihada zinazofanywa na TPSC za kumiliki majengo yao ambapo Kampasi ya Singida inaendelea na ujenzi wa majengo 30 na Kampasi ya Tanga majengo 15.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TPSC, Dkt. Florens Turuka amesema Bodi itaendelea kutoa ushauri ili Chuo kiendelee kuwa kinara katika masuala mbalimbali ikiwemo kujenga rasilimaliwatu yenye maadili, na yenye tija kwa taifa.

Akiwasilisha taarifa ya miaka 25 ya TPSC, Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Ernest Mabonesho amesema tangu kuanzishwa kwake, Chuo kimepata mafanikio makubwa katika maeneo mbalimbali ikiwemo taaluma, rasilimaliwatu na miundombinu.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!