Home Kitaifa KINANA ATIA SAINI KITABU CHA WAGENI, AZUNGUMZA NA VIONGOZI WA CCM GEITA.

KINANA ATIA SAINI KITABU CHA WAGENI, AZUNGUMZA NA VIONGOZI WA CCM GEITA.

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana, ametia saini kitabu cha wageni katika Ofisi za CCM Mkoa wa Geita na kuzungumza na viongozi wa Chama wa mkoa huo.

Kinana akizungumza na viongozi hao, amewataka kuendeleza ushirikiano uliopo ambao amesema ni nyenzo muhimu na msingi sahihi kwa maendeleo ya jamii.

Pia, amepongeza kazi kubwa inayofanywa na viongozi wa Chama na serikali mkoani humo huku akiwasisitiza viongozi na watendaji kuendelea kutatua changamoto za wananchi ili kuharakisha maendeleo.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!