Home Kitaifa SERIKALI YAMJIBU MATHAYO UCHAFUZI ZIWA VICTORIA

SERIKALI YAMJIBU MATHAYO UCHAFUZI ZIWA VICTORIA

Na Shomari Binda

SERIKALI imesema itaendelea kuhakikisha maziwa yote likiwemo ziwa Victoria yanakuwa katika usafi ili kutunza mazingira.

Kauli hiyo imetolewa bungeni hii leo na Waziri wa Muungano na Mazingira, Suleiman Jafo katika kipindi cha maswali na majibu.

Akiiibu swali la nyongeza la mbunge wa jimbo la Musoma mjini, Waziri Jafo amesema mazingira ya usafi kwenye maziwa yataendelea kuzingatiwa kupitia Wizara yake.

Waziri huyo amemuhakikishia mbunge Mathayo kuwa ziwa Victoria litaendelea kuangaliwa kimazingira ili wavuvi wakiwemo wa vizimba waendelee kufanya shughuli zao.

Akiuliza swali la nyongeza bungeni kwenye Wizara hiyo,mbunge wa jimbo la Musoma mjini,Vedastus Mathayo, alisema hivi karibuni ziwa hilo lilichafuka na kudaiwa ni kinyesi cha wanyama.

Mathayo katika swali lake amedai majibu hayo hsyakulidhishwa na wananchi na kutaka kujua udhibiti wa kimazingira wa ziwa hilo.

“Asante mheshimiwa Mwenyekiti kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza,hivi karibuni ziwa victoria lilichafuka na kupelekea samaki wakiwemo wanaofungwa kwenye vizimba kufa”

“Majibu ya serikali yalidai uchafuzi ule ulitokana na vinyesi vya wanyama lakini wananchi hawakulidhishwa na majibu yale” amesema Mathayo.

Kikao cha tatu katika bunge la 12 kimeendelea leo ambapo wabunge wamepata nafasi ya kuuliza maswali katika kipindi cha maswali na majibu.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!