Home Burudani SWAHILI FASHION  KUMFUNGULIA NJIA MUITALIANO GUIA

SWAHILI FASHION  KUMFUNGULIA NJIA MUITALIANO GUIA

Mbunifu wa Mavazi nchini Tanzania Guia Martinotti mwenye asili ya kitaliano akiwa kwenye jukwaa la ubunifu wa mavazi (Tanzania fashion festival) kwa mara ya kwanza lililoandaliwa na Mbunifu na mdau wa tasnia ya mitindo na ubunifu Deogratius kithama Jijini Dar es salaam

MBUNIFU wa Mavazi nchi ya Tanzania mwenye asili ya kitariano Guia martinotti amesema  ataendelea kufanya kazi za kibunifu nchini Tanzania kutokana na tasnia hiyo kupewa kipaumbele na wabunifu wengi waliopo nchini humo.

Martinotti ameeleza kwa namna miaka  05 ameishi nchini Tanzania  na kupokelewa na Mbunifu na mdau wa tasnia ya mitindo Deogratius kithama kwenye  Tamasha lake la mavazi nchini  (Tanzania fashion  festival) na kuona mwangaza wa kuendelea kunyanyua  kipaji chake kushiriki Matamasha makubwa ikiwemo swahili fashion week. 

“Watanzania wamekuwa nami bega kwa bega katika kuhakikisha napata nafasi ya kuonyesha bunifu zangu nchi Tanzania  akiwemo mdau wa tasnia ya ubunifu na mitindo Deogratius kithama kwenye jukwaa lake  pamoja na Mustafa Hassanali ambapo natarajia kushiriki jukwaa hilo  Disemba 02 mwaka huu kwa mara ya kwanza.”

Hata hivyo  amepongeza Muandaaji wa ‘swahili fashion week ‘ Mustafa Hassanali  kwa kuwapa nafasi wabunifu chipukizi kuonyesha bunifu zao pamoja na nchi zingine ambazo zinazungumza lugha ya Kiswahili kushiriki jukwaa hilo kwani inasaidia sana kubadilishana uzoefu baina ya wabunifu chipukizi na wakongwe pamoja na nchi na nchi .

Pia ameeleza shahuku yake kumvalisha Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mama Samia Suluhu nguo ambayo itaendana na  utamaduni wa kiafrika yenye mchanganyiko wa kitenge, khanga  pamoja na shuka la kamasai ili iweze kujitangaza Kimataifa nguo hiyo inayoitambulisha kwa namna moja au nyingine nchi ya Tanzania.

“Nigetamani kufanya bunifu ambayo angeweza kuvaa Rais wetu mpendwa na mchapakazi Mama Samia kutokana ni kiongozi ambae amekuwa mchapakazi na amefungua milango mingi ya fursa nchi Tanzania  pamoja na kuhakikisha anaiwakilisha na kutambulisha nchi ya Tanzania na vivutio yake hivyo kazi yetu wabunifu kuhakikisha tunatengeneza nguo zenye kuendelea kuitangaza nchi hii kwa mavazi mazuri yenye muonekano wa malighafi ya kitenge na khanga kutoka viwanda vilivyopo nchini humu

Miongoni mwa bunifu ambazo amefanya Mbunifu wa mavazi nchini Guia Martinotti mwenye asili ya kitaliano pichani ni nguo iliyotengenezwa na shuka la kimasai

..Mwisho.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!