Home Kitaifa NAIBU SPIKA ZUNGU ASHIRIKI KIKAO CHA KAMATI YA MAENDELEO ENDELEVU

NAIBU SPIKA ZUNGU ASHIRIKI KIKAO CHA KAMATI YA MAENDELEO ENDELEVU

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mussa Azzan Zungu ameshiriki Kikao cha Kamati ya Maendeleo Endelevu ambayo ni moja ya Kamati Sita za Bunge la Kimataifa linaloshughulikia masuala ya Uvumilivu na Amani (International Parliament for Peace and Tolerance).

Vikao vya Kamati hizo vimefanyika jana Jumatano tarehe 13 Julai, 2022 katika Bunge la Morocco vikitangulia Mkutano wa 10 wa Bunge hilo ambao utafunguliwa rasmi Alhamisi tarehe 14 Julai, 2022 na vikao vyake kumalizika tarehe 16 Julai, 2022.

Kauli mbiu ya mkutano huo ni ‘Securing food: a key prerequisite for Global Peace and Tolerance’

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!