Home Kitaifa RAIS SAMIA ANAVYOIMARISHA MIUNDOMBINU YA ELIMU KWA VITENDO

RAIS SAMIA ANAVYOIMARISHA MIUNDOMBINU YA ELIMU KWA VITENDO

Na Mwl Udadis, Temeke

Tangu alipoingia madarakani juhudi za Rais Samia katika kuboresha huduma kama vile Elimu, Afya na upatikanaji wa Maji safi na salama ni vipaumbele vilivyo wazi. Baadhi ya jitihada muhimu zilizofanyika ndani ya muda mfupi katika sekta ya Elimu ni pamoja na;

1. Ujenzi wa Shule mpya za sekondari na shule ya msingi zipatazo 266.

2. Ujenzi wa vyumba vipya vya madarasa ya shule za msingi, vituo shikizi, na shule za sekondari vipatavyo 18,219.

3. Ukamilishaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa shule za msingi na sekondari vipatavyo 4,525.

4. Ukamilishaji ujenzi wa vyumba vya maabara vipatavyo 1,399.

5. Ujenzi wa matundu ya vyoo kwa shule za msingi na sekondari yapatayo 568.

6. Ujenzi wa mabweni kwa shule za msingi na sekondari yapatayo 170.

7. Ujenzi wa nyumba za walimu wa shule za msingi na sekondari zipatazo 42.

8. Kutolewa ajira za walimu wapatao 9800 wa kada tofauti tofauti.

9. Watumishi katika wizara ya Elimu kwa maana ya walimu, waratibu wa Elimu na Maafisa Elimu kulipwa malimbikizo na madai yao yote yaliyohakikiwa.

10. Kutolewa fedha za Mikopo ya Elimu ya juu na kuondolewa kwa tozo ya VRF kiasi cha asilimia 6 kwa wanufaika wa Bodi ya Mikopo.

Rais Samia Suluhu anachapa kazi na anastahili pongezi za dhati kutoka kwa watanzania wote wenye mapenzi mema na nchi hii.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU MMBARIKI RAIS WETU

SisiTumekubali #Kaziinafanyika

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!