

Mbunge wa Vijana Mhe. Ng’wasi Damasi Kamani jana tarehe 23 Julai, 2023 alikabidhi pikipiki kwa Wilaya zote 7 za Mkoa wa Mwanza ikiwa ni sehemu ya mradi kwa vijana kujiwezesha na kujiinua kiuchumi.

Mhe. Ng’wasi amefanya hivyo ikiwa ni kuunga mkono adhma ya UVCCM Mkoa wa Mwanza kuwajengea uwezo vijana wa Mkoa huo kujiendeleza wenyewe badala ya kukaa mtaani bila kujishughulisha









