Home Kitaifa SANYA AISHUKURU JUMUIYA YA WAZAZI MARA KUMKUMBUKA, ATOA USHAURI

SANYA AISHUKURU JUMUIYA YA WAZAZI MARA KUMKUMBUKA, ATOA USHAURI

Na Shomari Binda-Musoma

MWENYEKITI wa zamani wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Mara Christopher Sanya ameishukuru jumuiya ya wazazi mkoa wa Mara kumualika kwenye baraza lake.

Licha ya kushukuru kualikwa kwenye baraza hilo la mkoa ametoa ushauri namna ya kupatikana kwa viongozi kupitia mikono ya wazazi.

Amesema jumuiya ya wazazi ni sehemu ya malezi hivyo kuna umuhimu mkubwa kupata kuona aina ya viongozi wanaotakiwa kuwaongoza wananchi.

Sanya amesema jumuiya ya wazazi inapaswa kupitia na kuona fomu za wagombea wanaoomba nafasi mbalimbali.

Naishukuru jumuiya ya wazazi mkoa wa Mara kwa kunikumbuka na kunikumbuka na mimi bado nipo sijastafu siasa na tutaendelea Kuwa pamoja”

“Jumuiya yetu imekuwa ikipanda na kushuka kutokana na aina ya viongozi wanaokuwa madarakani naamini waliopo kwa sasa mambo yatakwenda vizuri” amesema Sanya

Mwenyekuti wa Jumuiya ya Wazazi mkoa wa Mara,Kambarage Magubo,amemshukuru Sanya kwa kuendelea kutoa ushirikiano kwa Chama na jumuiya zake.

Amesema Sanya ni kiongozi mzuri ambaye jumuiya itaendelea kumtumia katika shughuli mbalimbali kwa kuwa ni kiongozi makini.

Akifungua baraza hilo la kwanza,Mjumbe wa Baraza la Wazazi Taifa na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Taifa Edwin Peter amesema jumuiya ya wazazi mkoa wa Mara inafanya vizuri miongoni mwa jumuiya Tanzania

Amesema vikao ndio umuhimu wa baraza na kuwaomba wajumbe kushirikiana na viongozi ili kuona mambo yanasonga na jumuiya kuimalika.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!