Home Kitaifa KATIBU UWT MUSOMA AWAHIMIZA WAGOMBEA WANAWAKE KUJIAMINI KWENYE KAMPENI

KATIBU UWT MUSOMA AWAHIMIZA WAGOMBEA WANAWAKE KUJIAMINI KWENYE KAMPENI

Na Shomari Binda-Musoma

KATIBU wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM Wilaya ya Musoma mjini Teddy Bageni amewahimiza wanawake kujiamini katika kipindi hiki cha kampeni.

Akizungumza na Mzawa Blog ofisini za jumuiya hiyo Teddy amesema kujimini kwenye kampeni kutawapa nafasi ya kumfikia kila mmoja kuomba kura.

Amesema wanachama wa CCM waliwaamini kwenye kura za maoni na kuwapa nafasi na kushinda na wanayo nafasi pia ya kushinda kwenye uchaguzi wa jumla.

Teddy amesema katika Wilaya ya Musoma mjini wapo wanawake waliosimama kuomba nafasi ya Mwenyekiti wa Mitaa na ujumbe na wana nafasi ya kushinda.

Amesema UWT Wilaya ya Musoma mjini kupitia viongozi wake kwa kushirikiana na wanachama wote watashiriki kampeni ya kuwaombea kura kwa wananchi.

Katibu huyo amesema wamejipanga vizuri katika siku 6 za kampeni kuomba kura na kuweza kufikia lengo

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!