Home Kitaifa MRADI WA MAJIKO BANIFU WATAMBULISHWA GEITA .

MRADI WA MAJIKO BANIFU WATAMBULISHWA GEITA .

Serikali ya Mkoa wa Geita kupitia Kaimu katibu tawala wa mkoa wa Geita ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya Mipango na Uratibu, Ndugu Deodatus Kayango leo Februari 02, 2026 imepokea mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku.

Akizungumza wakati wa utoaji wa taarifa ya mradi, Mhandisi Mwandamizi kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Deusdedit Malulu amesema,

Serikali kupitia REA imekuja na mpango wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku ambao utasaidia kupunguza athari za kiafya na mazingira zitokanazo na matumizi ya nishati isiyo salama ya kupikia.

Aidha, usambazaji na uuzaji wa majiko haya banifu ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa matumizi ya nishati safi ya kupikia wenye dhima mpaka ifikapo mwaka 2034 zaidi ya asilimia themanini 80% ya watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia.

Halikadhalika, katika kufanikisha hilo Wakala wa Nishati Vijijini unatarajia kusambaza na kuuza majiko banifu katika wilaya zote tano za mkoa wa Geita ambapo kwa wilaya za Mbogwe, Chato, Geita na Nyang’wale zitapata majiko 2,105 na wilaya ya Bukombe majiko 2,106.

Aidha, mkataba wa mradi huu ulisainiwa kati ya REA na mtoa huduma Kampuni ya Geita Millenium Star Company Limited na utatekelezwa ndani ya miezi 15 ambapo mtoa huduma atasambaza na kuuza kwa bei ya ruzuku majiko banifu 8,486.

Aidha, gharama ya mradi ni zaidi ya TZS Milioni 385.7 ambapo serikali itatoa ruzuku ya asilimia themanini na tano (85%) sawa na zaidi ya TZS Milioni 327.9 hivyo badala ya jiko kuuzwa kwa bei ya awali ya TZS 35,000 litauzwa kwa bei ya ruzuku ya TZS 29,750 na mwananchi atachangia TZS 5,250 tu.

Aidha, ndugu Kayango ameipongeza REA kwa kuendelea kutekeleza kwa vitendo maono ya Mhe. Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha mwananchi anakuwa na uwezo wa kutumia na kupata nishati safi na salama ya kupikia yenye ufanisi mkubwa, rahisi na nafuu kupatikana.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!