.
Afisa Mkuu wa Tigo Business, Bw. John Sicilima akimkabidhi Mjasiriamali router ya 5G, katika uzinduzi wa Mjasiriamali box iliyoboreshwa kwaajili ya wajasiriamali na wafanyabiashari wadogo wadogo na wa kati (SMEs).
Na Mwandishi Wetu.
Dar es Salaam, 14 Novemba 2024 – Tigo Tanzania kupitia kitengo chake cha Tigo Business leo imetangaza uzinduzi wa toleo jipya na lililoboreshwa la Mjasiriamali Box, kifurushi maalum kinacholenga kusaidia Wajasiriamali na Biashara Ndogo ndogo na za Kati (SMEs) kote nchini. Mjasiriamali Box 2.0 inakuja na huduma mpya na zana muhimu kwa ajili ya kurahisisha shughuli za biashara, usimamizi wa fedha, na kusaidia ukuaji wa biashara katika ulimwengu wa kidigitali.
Mjasiriamali Box inawapa wajasiriamali na SMEs kifurushi chenye router za 5G kwa ajili ya mtandao wa kasi, jukwaa la Usimamizi wa Fedha kwa ufuatiliaji wa mapato na matumizi, pamoja na Portal ya Mjasiriamali Box inayounganisha huduma zote kwa urahisi mahali pamoja. Kupitia msaada wa Tigo, sasa wajasiriamali wa Tanzania wanaweza kupata huduma hizi zote kwa sehemu moja, bila ya kuhitaji kuhangaika kwa watoa huduma tofauti.
Akizungumza katika uzinduzi huo, John Scilima, Afisa Mkuu wa Tigo Business, alisema, “Biashara nyingi ndogo ndogo zinapata changamoto ya kupata huduma tofauti kwa ajili ya mtandao, huduma za kifedha, na mawasiliano. Mara nyingi zinapaswa kwenda kwa watoa huduma mbalimbali, jambo linalochukua muda, na kuongeza gharama. Kupitia Mjasiriamali Box iliyoboreshwa, Tigo Business inatoa suluhisho moja linalowapatia kila kitu wanachohitaji kwa urahisi.”
Mjasiriamali Box iliyoboreshwa pia inajumuisha mikopo ya biashara kuanzia TZS 120,000 hadi TZS milioni 2, ili kuwasaidia wajasiriamali wanaotaka kuongeza mteja wa biashara zao au kutimiza mahitaji yao ya kila siku. Pamoja na zana za masoko ya kidigitali na mawasiliano, kifurushi hiki kinawawezesha kuwafikia wateja kwa urahisi zaidi.
Scilima aliongeza kuwa, “Mjasiriamali Box ni zaidi ya mtandao – ni msaada wa kweli kwa wajasiriamali kusimamia fedha zao, kuwasiliana vizuri, na kupata taarifa muhimu za biashara. Kupitia Portal ya Mjasiriamali Box, wamiliki wa biashara wanaweza kuona maendeleo yao na kusimamia shughuli zao zote kwa urahisi.”
Kwa bei ya kuanzia TZS 120,000, Mjasiriamali Box 2.0 ni suluhisho nafuu linaloweza kutumiwa na biashara za aina zote. Tigo inaendelea kuonyesha dhamira yake ya kukuza biashara za Tanzania na kuleta ubunifu kwenye sekta ya biashara.
Wajasiriamali wanaotaka kujua zaidi kuhusu Mjasiriamali Box 2.0 wanaweza kutembelea maduka ya Tigo au kuwasiliana na huduma kwa wateja kwa maelezo zaidi.











Nilisoma maelezo kuhusu mikopo ya simu kuwa inaanzia tsh 35000 kisha kisha mrejesho kwa siku ni tsh 600 kwa muda wa mwaka mmoja. Nilikwenda tigo shop Tabora mkabala na msikiti wa ijumaa Gongoni tabora walikataa Kanipa na pesa nilikuwa nayo
Hawawezi kukukatalia, labda haukuwa umekidhi vigezo vya kupewa mkopo wa hiyo sim
I read information about mobile
loans that starts Tsh 35000 and
then a day’s return is Tsh 600 for
one year. I went to Tigo Shop
Tabora opposite the Mosque on
Friday Gongoni Tabora refused to
give me the money I had the
amount they mentioned. After
calling the number 100 they said
the phones were there if they were
gone they would have provided
information.
I read information about mobile loans. Being starts with Tsh 35000. Then the day’s feed is Tsh 600 for one year. I went to Tigo Shop Tabora. With the mosque on Friday Gongoni Tabora refused to give me the phone while the money I had in the amount they mentioned. Criteria I had. If I have a National ID, I have used a phone card for at least three months. After calling the number 100 customer service they said the phones were available. If they were gone they would give information.