Home Kitaifa DKT.HOMERA AWASILI NCHINI USWISI  KUHUDHURIA MKUTANO WA BARAZA LA HAKI ZA BINADAMU...

DKT.HOMERA AWASILI NCHINI USWISI  KUHUDHURIA MKUTANO WA BARAZA LA HAKI ZA BINADAMU LA UMOJA WA MATAIFA

Waziri wa Katiba  na Sheria Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera amewasili Nchini Geneva, Uswisi kuhudhuria Mkutano wa Ngazi ya Juu katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa linaloanza leo tarehe 23 Februari, 2026. 

Katika kikao hicho, Mhe. Waziri anatarajia kuwasilisha taarifa ya Nchi juu ya hali ya Haki za Binadamu nchini.

Awali Mhe. Homera ametembelea Ofisi za Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania nchini Geneva ambapo amekutana na kufanya mazungumzo na 

Balozi na Dkt. Abdallah Possi ambaye ni Mwakilishi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Ofisi za Umoja wa Mataifa na Balozi na Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Umoja wa Mataifa Dkt. Hoyce Temu.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!