
Bw. Kawawa Luduko ni Mkulima Maharufu Wa kilimo Cha Pamba Mkoani Geita Kijiji Cha Bukwimba Wilaya ya Nyang’nwale Mkoani ameeleze jinsi kilimo Cha Pamba kilivyompatia faida na kiwango chake cha Elimu ni darasa la saba ameoa Mke na watoto 10 na wote Wana Elimu.
Akizungumza na Mzawa blog amesema Mwaka 2011 alipata tuzo ya Ukulima Bora wa kilimo Cha Pamba ambapo kikao hicho Cha kitaifa kilichowakutanisha wakulima na wadau wa Pamba nchini ilikuwa ni Fursa ya yeye kumsaidia na kujifunza mengi pia kubadilishana mawazo na watu Mbalimbali waliokuwa kwenye kikao hicho, “huo Ndio ulilokuwa Mwanzo wa kufungua Milango yangu nimejenga Nyumba mbili na Nyumba za Biashara nimesomesha lakini pia ninalima mazao Mengine kama Mahindi Mpunga na dengu kilimo kikubwa Kwangu ni kilimo Cha Pamba” alisema Bw. Luduko
Aidha ameiomba Serikali Kuleta Mbolea Mapema, pamoja na Viwatilifu Ili aweze kufanya Vizuri. “mpaka Sasa nipo kwenye mahandalizi ya kuhakikisha nafanya Vizuri kama Mwaka 2011 na nitafata kanuni zote za kilimo Cha Pamba” amesema Bw. Luduko
Hata hivyi Bw. Ludoku ameipongeza TCB Kwa usimamizi wao mzuri wa dhao la Pamba chini ya Serikali yetu Makini inayoongozwa na Mhe. Rais. Dkt Samia Suluhu Hassan. “naiomba serikali itusaidie tuweze kupata Mikopo ya kutusaidia kwenye Kilimo Cha Pamba maana kina Kazi nyingi na kubwa na kinaitaji huangalizi na kupaliliwa Mara Kwa Mara” amesema








