Na Magrethy Katengu
Wakala wa Usajili wa biashara na lessni BRELA Wameshukuru waliowapigia kura hadi kupata tuzo tatu ambazo ya kwanza ni tuzo ya Udhamini, Uwezeshaji masuala ya Uwekezaji na Uwezeshaji biashara , Banda bora la washiriki mwaka huu
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kupokea tuzo hizo kutoka kwa Rais wa Zanzibar Ally Hassan Mwinyi Wakati akifunga mainyesho ya 47 ya Sabasaba Jijini Dar es salaam Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu Brela Andrew Mkapa ameshukuru wafanyakazi wote wa Brela kwa maana tuzo zote zimepatikana kwa sababu ya michango yao .
“Kwani hauwezi kupata tuzo hizi mtu mmoja pasipokuwa michango yao hivyo nawapongeza na kusisitiza kuwa tuendelee kufanya hivi hata katika maonyesho yajayo kama timu ili tuendelee kuonyesha umahiri wetu kwa ushiriki wa sabasaba” amesema Andrew









